"Leo tunawapa vyandarua tunaomba mkavitumie kujikinga na Malaria. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hataki kuona mwananchi wake anapoteza maisha kwa sababu ya Malaria ndiyo maana ameleta vyandarua na Madaktari"
Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mhe. Onesmo Buswelu (kulia) akifuarahi na Diwani wa Kata ya Bulamata baada ya kuweka Jiwe la Msingi kituo cha Afya Bulamata.
Mkuu wa wilaya akimkabidhi chandarua mama mjamzito kama sehemu ya Serikali kuwakinga Wananchi wake dhidi ya Malaria.
Awali Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Tanganyika, Dkt. Alex Mrema alimweleza Mkuu wa Wilaya kuwa Serikali imeleta vifaa kwa ajili ya mama wajawazito ikiwemo vyandarua ambavyo vitakawiwa bure.
Baadhi ya wananchi waliofika kupata huduma katika kituo hicho wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea kituo cha Afya karibu kwani mwanzo walikuwa napata shida kufuata huduma maeneo ya mbali.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment