Wednesday 11 July 2018

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MHE. DKT. HAMISI KIGWANGALA KATIA TIMU HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA


 WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MHE. DKT. HAMISI KIGWANGALA KATIA TIMU HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA



Msitu wa Tongwe Magharibi kuwanufaisha wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Wataalam kutoka ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda wakiomuonesha ramani waziri wa maliasili na utalii juu ya vijiji vinavyozunguka msitu huo.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MHE. DKT. HAMISI KIGWANGALA KATIA TIMU HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MHE. DKT. HAMISI KIGWANGALA KATIA TIMU HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA.

Waziri wa maliasili na utali Mhe. Dkt. Hamis Kigwangala (wa pili kutoka kulia. Anayefuata kutoka kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda, Bw. Romuli Rojas John, Mkuu wa wilaya ya Tanganyika, mhe. Salehe Mhando na afisa wanyama pori Churchward.

waziri wa Maliasili na utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangala katia timu Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda



waziri wa Maliasili na utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangala katia timu Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda




Waziri wa maliasili na utalii Mhe. Dkt. Hamis Kigwangala akiteremka kutoka kwenye maporomoko ya Nkondwe yanayopatikana katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Waziri Kigwangala amefanya ziara ya kutembelea na kukagua misitu ya Tongwe Mashariki na Magharibi Julai 09, 2018.




Mkurugenziwa Mpanda DC akisalimiana na waziri wa Maliasili na utalii



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda akisalimiana na waziri wa Maliasili na utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangala. Dkt. Kigwangala amefanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Julai 09, 2018.



Waziri wa maliasili na utali afanya utalii Nkondwe



Posted On: July 10th, 2018
Halmashauri ya wilaya ya Mpanda imepongezwa kwa kutunza na kuhifadhi misitu ya Tongwe mashariki, Nkamba na misitu ya vijiji.
Pongezi hizo zimetolewa na waziri wa maliasili na utalii mhe. Dkt Hamis Kigwangala, Julai 09, 2018 alipofanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda (Tanganyika). Baada ya kupokea taarifa iliyowasilishwa na Mkuu wa wilaya ya Tanganyika mhe. Salehe mhando, taarifa hiyo ilisheheni  fursa za utalii zinazopatikana katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda na umahili mkubwa wa kuhifadhi misitu.
Fursa hizo ni pamoja na eneo la Karema linalopatikana katika mwambao wa ziwa Tanganyika ambapo Daktari wa kwanza mwafrika aliishi pale na kuzikwa Karema.
Hata hivyo, Dkt. Kigwangala alioneshwa eneo la uwekezaji lenye ukubwa wa hekta 46,000 ambapo kuna eneo lililotengwa kwa ajili ya  utalii ikolojia. Eneo hilo la utalii ikolojia lina maporomoko mazuri katika mlima wa Nkondwe, sokwe mtu, vipepeo vya rangi za kipekee na vivutio vingi vya kitalii.
Baada ya kufika katika maporomoko hayo, msafara ulielekea katika msitu wa Tongwe Mashariki ambao unamilikiwa na kulindwa na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Baada ya kujionea kwa macho namna msitu ulivyofunga na kulindwa kwa umakini, msafara ulielekea katika msitu wa Tongwe Magharibi.
Msitu wa Tongwe Magharibi umezungukwa na vijiji 11 vya Halmashauri ya wilaya ya Mpanda. Halmashauri ya wilaya ya Mpanda imeomba kukabidhiwa msitu huo wa Tongwe Magharibi kwani ina uwezo wa kuulinda na kuuhifadhi. Msitu wa Tongwe Magharibi ni chanzo cha mito 16 inayotiririsha maji yake katika Halmashauri ya wilaya ya Mpanda na mjawapo wa mito hiyo ni pamoja na mto Katuma na Mnyamasi.
Halmashauri ya wilaya ya Mpanda kwa kushirikiana na wadau wa utunzaji wa mazingira hasa Taasisi ya Jane Goodall, Tuungane na FZS wamekuwa wakisaidia sana kutoa fedha za kufanya matumizi bora ya ardhi. Hadi sasa vijiji 23 kati ya 55 vimefanya matumizi bora ya ardhi.
Aidha, wananchi wameelimishwa vya kutosha juu ya utunzaji wa mazingira hasa misitu na vijiji 9 vinatarajia kuingia katika makubaliano ya kuuza hewa ya ukaa muda wowote kuanzia sasa.

Monday 9 July 2018

HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA (TANGANYIKA) YAITENDEA HAKI MAADHIMISHO NA SIKUKUU YA SABASABA TAREHE 07-07-2018




Mwnyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda (Tanganyika) Mhe. Hamadi Mapengo akitoa vyeti kwa mkuu wa gereza la Kalilankulu pia alitoa vyeti vya shukrani kwa tasisi mbalimbali na mashirika yaliyochangia na kujitolea kwa hali na mali katika maandalizi ya kuukaribisha Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Mpanda (Tanganyika) yote haya yalifanyika siku ya sikuku na maadhimisho ya Sabsaba 07-07-2018

HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA (TANGANYIKA) YAITENDEA HAKI MAADHIMISHO NA SIKUKUU YA SABASABA TAREHE 07-07-2018


Mhe. Hamadi Mapengo Mwnyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda akimkabizi Ngao na kiasi cha shilingi laki moja nahoza wa timu ya Kabungu FC kama zawadi ya mshindi wa kwanza na mkuu wa wilaya ya Mpanda Mhe. Salehe Mhando na Mkurugenzi Mtendaji Bw. Romuli R. John.





Wafanyabiashara wlijitokeza na kufanya biashara bila kuwasahau wajasiriamali kwani hawakuachwa nyuma walileta bidhaa zao


 
Mpambano mkali zidi ya Kabungu FC na Mchakamchaka FC,  Kabungu FC ilifanikiwa kuibuka kidedea kwa kuicharaza Mchakamchaka FC kw mikwaju ya penati 5-4 baada ya kutoka droo ya 2-2 uwanjani.
 
 
Sikukuu na maadhimisho ya Sabasaba katika Halmashuri ya Wilaya ya Mpanda (Tanganyika) imekuwa ya mafanikio makubwa kwa wafanyabiashara kwani wameweza kuongea na kutoa maoni yao juu ya maswala ya kibishaka katika Wilaya ya Mpanda (Tanganyika), baada ya kuongea na mkuu wa wilaya Mhe.Salehe Mhando akiwa amejumuika na Mhe. Hamadi Mapengo Mwnyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda na Mkurugenzi Mtendaji Bw. Romuli R. John