ZAIDI YA NYUMBA KUMI ZIMEATHIRIKA KUTOKANA NA MVUA
Zaidi ya nyumba kumi zimeathirika kutokana na mvua
iliyonyesha juzi ikiwa imeambatana na upepo mkali katika kijiji cha kabungu
Kata ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika na kusabaisha familia nane kukosa makazi
na kuhifadhiwa na wasamalia wema.
Akitoa taarifa ya
athari za mvua hiyo mbele ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya iliyoongoza
na kamati kamati ya maafa Afisa taarafa wa Tarafa ya Kabungu Odes Gwamaka
ameleza kuwa baada ya kupokea taarifa hizo uongozi wa serikali ya kijiji kata
na Tarafa walifika eneo la tukio kuwajulia hali wahanga na kuchukua hatua za haraka kuwapa msaada wa
kibinadamu ikiwa ni pamoja na kuwatafutia mahali pa kulala kwa wale
walioezuliwa nyumba zao.
Mkuu wa Wilaya ya
Tanganyika Salehe Mhando ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na
usalama na kamati ya maafa ya wilaya ametembelea wahanga na kuwapa pole na msaada ya awali ya
kibinadamu kama chakula,na kutoa maaelekzeo tathimini ifanyike mapema ili kujua
hasara iliyopatikana
Aidha amewaelekeza wananchi wanapojenga nyumba waepuke ile
tabia iliyozoelekea ya kutokufunga lenta ,kwani nyumba yenye lenta inakuwa
imara Zaidi,na kusisitiza kupanda miti kwenye maeneo yao kwa kuwa inasaidia
kupunguza kasi ya upepo pindi mvua
zinaponyesha zhasa zile za upepo mkali.
Kwa Upande wake Katibu
wa Kamati ya maafa ya wilaya ya Tanganyika
Reginald Mhango ambaye pia ni Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya kwa kushirikiana na uongozi wa Kijiji
,Kata na Tarafa ametoa mchanganua wa msaada uliopatikana na jinsi utukagawiwa kwa walengwa,ambapo kwa
harakahara vitu vilivyolewa unga wa sembe,maharage,sabuni sukari vinathamani ya
Zaidi ya shilingi laki tano kwa kuthamanisha.
Diwani wa Kata ya Kabungu Christina Reonard Sanane
ameshukuru kwa niaba ya wananchi wake kwa msaada wa awali uliotolewa na
serikali sanjari na kuwahifadhi wahanga walioathiliwa na mvua hizo kwa
kubomolewa numba zao.
Wananchi wamepewa tahadhari kuwa waangalifu kutokana na Mvua
zilizoanza kunyesha maeneo mbalimbali nchini ambazo zimeanza kuleta madhara.
No comments:
Post a Comment