Friday 26 May 2023

DC BUSWELU AHIMIZA UKWELI KWENYE MAENDELEO AMBAYO SERIKALI INAYAFANYA

MKUU wa wilaya ya Tanganyika Mhe. Onesmo Buswelu

Mkuu wa kituo cha Polisi wilaya ya Tanganyika, ACP Kiberiti

MKUU wa wilaya ya Tanganyika Mhe. Onesmo Buswelu ametoa wito kwa watanzania kuwa wakweli katika maendeleo ambayo Serikali inayafanya pasipo kupotosha.

DC Buswelu ametoa wito huo baada ya kutembelea na kukagua hatua ya ujenzi wa kituo cha Polisi Tanganyika, ambapo amsema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha mazingira ya Askari Polisi wilayani humo ikiwemo kuwajengea nyumba Watumishi wa Jeshi hilo.

Hayo yamejiri baada ya kauli ya Katibu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Salumu Mwalimu akiwa ziarani wilayani humo kutoa kauli ambayo siyo ya kweli kuwa OCD hana nyumba ya kuishi wakati viongozi wengine wamejengewa nyumba na Serikali.

"kuna nyumba kubwa imeshakamilika three in one. Polisi hawajasahaulika na kazi inaendelea vizuri wapo ambao tayari wameshahamia kwenye nyumba zile, nyumba zina maji na umeme"

Nyumba ya watumishi wa Jeshi la Polisi (Three in One)

Aidha, DC Buswelu amesema licha ya kukamilisha ujenzi wa nyumba hizo, Serikali inajenga kituo cha kisasa cha Polisi kitakacho ghalimu shilingi milioni 500 ambapo ujenzi wake umefikia hatua ya kumwaga jamvi.

Kwa upande wake Mkuu wa kituo cha Polisi wilaya ya Tanganyika, ACP Kiberiti amesema kwa kiasi kikubwa uwepo wa nyumba hizo umesaidia wananchi kupata huduma ya kiusalama haraka.

ACP Kiberiti ameongeza kuwa, ujenzi wa kituo cha  Polisi ulisimama kutokana na mvua zilizokuwa zikinyesha kutokana na jeografia ya wilaya hiyo hivyo ujenzi utaendelea hivi karibuni.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment