Serikali yatoa Mil. 900 vituo vya afya Mwese, Mishamo
Serikali ya awamu ya 5 imeleta neema ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya vya Mishamo na Mwese. Kituo cha afya cha Mishamo kimepata milioni 400 za kujenga wodi ya kina mama, chumba cha kuhifadhia maiti, maabara, sehemu ya kuchomea taka ngumu na miundombinu mingine inayohusiana na afya.
Ujenzi wa kituo hicho unaenda vizuri na sasa umefikia katika hatua za umaliziaji. Wananchi wamejitoa sana katika kusomba mawe na matofali.
No comments:
Post a Comment