Wednesday 23 May 2018

Serikali yatoa Mil. 900 vituo vya afya Mwese, Mishamo

Serikali yatoa Mil. 900 vituo vya afya Mwese, Mishamo

Serikali ya awamu ya 5 imeleta neema ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya vya Mishamo na Mwese. Kituo cha afya cha Mishamo kimepata milioni 400 za kujenga wodi ya kina mama, chumba cha kuhifadhia maiti, maabara, sehemu ya kuchomea taka ngumu na miundombinu mingine inayohusiana na afya.
Ujenzi wa kituo hicho unaenda vizuri na sasa umefikia katika hatua za umaliziaji. Wananchi wamejitoa sana katika kusomba mawe na matofali.
Wakati kituo cha afya cha Mwese kimepata shilingi milioni 500 na tayari zimeshaingia katika akaunti ya kijiji tangu Mei 9, 2018. Wananchi wa kata ya Mwese wameshaweka mikakati ya kuhakikisha ujenzi na ukarabati wa nyumba 9 za wahudumu wa afya zinakamilika mapema.


No comments:

Post a Comment