Wednesday 8 March 2023

KATAVI: CHUO CHA VETA KUJENGWA WILAYANI TANGANYIKA, EKARI 20 ZATENGWA.

HALMASHAURI ya wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi imetoa ekari 20 kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Wilayani Tanganyika.

Akizungumza walipokwenda kulitembelea eneo hilo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Shaban Juma amesema kama Halmashauri imejipanga kuhakikisha chuo hicho kinajengewa.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Shaban Juma.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu amesema watahakikisha wanasimamia ujenzi kwa kuwa kuna Vijana wengi ambao walio hitimu darasa la saba na kidato cha nne hivyo kukamilika kwa chuo hicho itakuwa mkombozi kwa Vijana wengi wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kusini Magharibi, Shomari Omary amesema wameamua kujenga chuo hicho Tanganyika baada ya kugundua kuna uhitaji mkubwa.

Omary amesema wameridhishwa na mandhari ya eneo hilo na mikakati ya ujenzi itaanza mwishoni mwa mwezi huu endapo watapata hati miliki ya eneo hilo.

Kaimu Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kusini Magharibi, Shomari Omary.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tanganyika Hamad Mapengo ameishukuru Serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA).

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tanganyika Hamad Mapengo.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment