Friday, 17 February 2023
WATUMISHI NA WATENDAJI TANGANYIKA WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI.
Thursday, 16 February 2023
RC KATAVI AAGIZA KUCHUKULIWA HATUA KALI WAZAZI AMBAO HAWAJAWAPELEKA WATOTO KUANZA MASOMO.
MKUU wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Hoza Mridoko ameagiza kuchukuliwa hatua kali za kisheria kwa wazazi ambao bado hawajawapeleka watoto kuripoti kidato cha kwanza.
Sunday, 12 February 2023
RC MRINDOKO AKOSHWA NA MRADI ULIOTEKELEZWA KWA FEDHA ZA HEWA UKAA.
MKUU wa Mkoa wa Katavi Mhe.Mwanamvua Mrindoko ameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa nyumba ya Walimu yenye uwezo wa kubeba watumishi wawili iliyojengwa kwa Fedha za hewa ukaa katika Kijiji cha Lwega Kata ya Mwese Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.

Mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Mpembe Kata ya Katuma unaotekelezwa kupitia fedha za mradi wa hewa ukaa.
Saturday, 11 February 2023
CCM TANGANYIKA YAAHIDI USHIRIKIANO KUFIKIA MALENGO YA KUKUSANYA BILIONI 40.3
MWENYEKITI wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi Yasin Kiberiti amesema hana wasiwasi na halmashauri ya Tanganyika kufikia na hata kuzidi lengo la kukusanya na kutumia Tsh. Bilioni 40.3 endapo vyanzo vya mapato vitasimamiwa vizuri.
Wednesday, 8 February 2023
HALMASHAURI YA TANGANYIKA KUKUSANYA TSH. BILIONI 40.3 MWAKA WA FEDHA 2023/24.
PICHA: Kushoto ni Mwenyekiti wa Kikao cha kamati ya ushauri Wilaya (DCC) Wilaya ya Tanganyika ambaye pia ni mkuu wa wilaya Onesmo Buswelu akiteta jambo na Mkurugenzi mtendaji Juma Shabani (mwenye miwani) pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tanganyika Hamad Mapengo.
HALMASHAURI ya wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/24 inatarajia kukusanya na kutumia kiasi cha Tsh. Bilioni 40.3, ikiwa ni ongezeko la asilimia 23.5 ya bajeti ya mwaka 2022/23 ya Tsh. Bilioni 32.6
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tanganyika Juma Shaban leo Februari 8, 2023 alipokuwa akiwasilisha taarifa ya rasimu ya bajeti mbele ya wajumbe katika Kikao cha kamati ya ushauri Wilaya (DCC) Wilaya ya Tanganyika kilichoongozwa na mwenyekiti wake ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkurugenzi.
Mkurugenzi huyo amesema chanzo cha bajeti hiyo kuongezeka ni kutokana na kuongezeka kwa makisio ya mishahara ya Watumishi, vyanzo vya mapato hasa chanzo cha mrahaba unaotokana na hewa ukaa, uuzaji wa Viwanja, kuongezeka kwa mazao ya kilimo na kutokana na kukua kwa biashara ya mazao ndani na nje ya Nchi.
Amesema Halmashauri hiyo imepanga kukusanya kiasi hicho cha fedha kutoka katika vyanzo mbalimbali vya mapato ikiwemo mapato ya ndani, fedha za ruzuku kutoka Serikali kuu na ruzuku kutoka kwa wafadhili na wahisani.
"Kwanza tuna mapato ya ndani ambayo yana jumla ya Bilioni 10 ambayo bajeti hii imeongezeka ukilinganisha na bajeti ya mwaka uliopita, kutokana na kuongezeka kwa bajeti matumizi mengineyo ni asilimia 40 na miradi ya maendeleo itakuwa asilimia 60"
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tanganyika Juma Shaban akiwasilisha mpango wa rasimu ya bajeti kwa Mwaka wa fedha 2023/24 katika kikao cha DCC kilichofanyika leo katika Ukumbi wa mikutano wa Mkurugenzi.
Aidha ameongeza kuwa "kuna chanzo ambacho ni fedha za hewa ukaa ambazo hizi ni mapato fungiwa kwa sababu fedha hizi zinaenda moja kwa moja kwenye Vijiji husika ambapo imekadiriwa kupokea Bilioni Nne na Milioni mia mbili na kumi na mbili elfu"
Amesema bajeti hiyo imezingatia kukamilisha ujenzi wa miradi ya maendeleo iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ikiwemo kuimarisha sekta ya afya, elimu na Maliasili.
Mikakati mingine ni kujenga shule ya mchepuo wa kingereza (English medium) ili kutatua tatizo la aina hiyo ya shule katika Halmashauri, kuboresha kituo cha Afya Sibwesa kuwa cha mfano, kuboresha Hospitali ya Ikola na kuanzisha kituo cha nyuki cha kuchataka asali sambamba na kukarabati nyumba zipatazo 14 za Halmashauri zilizopo Mpanda mjini ukiwemo ukumbi wa Idara ya Maji.
Katika sekata ya Maji akiwasilisha rasimu ya bajeti Mhandisi wa Wakala wa Usambazaji wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Tanganyika Festo Mpogole amesema katika mwaka wa fedha 2023/24 RUWASA wilayani Tanganyika imepanga kutumia Tsh. Bilioni 1.6 kutekeleza miradi mbalimbali ya maji.
Nae mwakilishi kutoka Wakala wa Barabara za mijini na vijijini (TARURA) wilaya ya Tanganyika Mhandisi Bonventure Katambi amesema jumla ya Tsh. Bilioni 4.7 zinatarajiwa kutumika katika matengenezo ya barabara wilayani humo.
PICHA ya kwanza ni Mhandisi wa Wakala wa Usambazaji wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilaya ya Tanganyika Festo Mpogole na Picha ya pili ni Mhandisi Bonventure Katambi kutoka Wakala wa Barabara za mijini na vijijini (TARURA) wilaya ya Tanganyika wakiwasilisha taarifa.
Akihitimisha Kikao hicho, Mwenyekiti wa kikao ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Onesmo Buswelu amehimiza kupanga mipango mathubuti ya ukusanyaji mapato ili kufikia adhima ya utekelezaji wa miradi.
Aidha, ametumia kikao hicho kutoa wito kwa Watumishi kutimiza wajibu wao kwa kuchapa kazi na kuzingatia ufanisi huku akiwaomba Viongozi wa Dini kuwaombea Viongozi ili waweze kutimiza majukumu yao ya kuwatumikia wananchi.
Mwenyekiti wa Kikao cha kamati ya ushauri Wilaya (DCC) Wilaya ya Tanganyika ambaye pia ni mkuu wa wilaya Onesmo Buswelu akitoa maelekezo wakati akifunga kikao.
Rasmu hiyo ya bajeti inatarajiwa kusomwa na kupitishwa katika kikao cha bajeti cha baraza la madiwani siku ya Ijumaa tarehe 10 Februari 2023.
MWISHO.
Sunday, 5 February 2023
RC KATAVI ATAJA MAFANIKIO YA MKOA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 46 YA CCM.
UJUMBE WA CCM MKOA WA KATAVI KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 46.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Comred Idd Kimanta,mgeni rasmi katika maadhimisho ya Miaka 46 ya CCM.